Zabron Singers – Nitasubiri Lyrics

Zabron Singers Nitasubiri Lyrics

Zabron Singers – Nitasubiri Lyrics

Nitasubiri Lyrics by Zabron Singers

Ya nini Mungu kujificha wakati wa shida?
Wakati mwingine kama kweli huoni
Wajua yote yalonikuta hasimliki
Nimelia na kujinyamazisha pekee yangu

Moyoni nikataabika, furaha ikaenda
Sikumwona wa kumwelezea shida
Rafiki pekee namwamini, ni Yesu mfariji
Ndio maana sijamwambia mtu shida zangu

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Kwa nini sasa umesimama mbali nami Bwana?
Muda mwingi mi najihisi mi ni mpweke
Jidhihirishe mi nikuone, nakuhitaji Bwana
Nibariki sasa ukijibu maombi, yangu

Najua mengi nimekuudhi, nimetenda dhambi
Ndio maana ukasimama mbali nami
Nisamehe yote yote bure, kwa damu ya Yesu
Nifanye mi niwe mtoto wako siku, zote

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Nitasubiri na kusubiri sitachoka
Nimeshamezana na wewe kwa maombi
Usipojibu, au ujibu nitaelewa
Nashukuru, hata kwa majaribu
Mungu unasababu mimi kuishi maisha kama haya

Written by; Zabron Singers
Released date; 18 January, 2021

Zabron Singers Nitasubiri Lyrics